Saturday 17 August 2013

MWANASHERIA MKUU SMZ ” SERIKALI 2 NI KUVUNJA MUUNGANO

Na Salim Salim
Mwanaseria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi wa Zanzibar leo amesema lengo la kuandikwa kwa Katiba Mpya si kuyafanyia Marekebisho katiba iliyokuwepo sasa bali ni kandika Katiba Mpya katiba ambayo itakuwa Muarubaini kwa kero za Muungano na Muungano wenyewe. Mwanaseheria Mkuu liyasema hayo leo asubuhi alipokwa akifunguwa Baraza la Katiba la Vyuo Vikuu liliondaliwa na ZAHILFE Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Zanzibar liliofanyika katika Ukumbi wa Salama Hal Bwawani.
Alilisifu Baraza hilo na kusema kuwa ni Baraza la Vijana wasome na kuwasifu Vijana kwa ile sifa yao kubwa ya kuleta mapinduzi katika jamii yeyote.Alimtaja kijana Sir King ndie waliosababisha Zanzibar iiteme Tanganyika mwaka 1895 Ogast na Tanganyika kuangukia katika mikono wa Wajerumani. Na kumtaja Gerald Pota alietumwa na Waingereza kuja kuunda Serikali na kumpangia Mfalme mshahara ambako alikuwa akilipwa paund 250 kwa mwaka. Msingi wa Muungano wa Tanzania ni kuungana kwa Nchi mbili huru Tanganyika na Zanzibar lengo la kuungana kwa nchi mbili hizi ni kufanya mambo yao pamoja na kupata faida zaidi na sio Nchi moja kuitawala Nchi nyengine alisema, hukua akiendela kusema:
Zanzibar si mkowa wala wilaya, Zanzibar ni Nchi, katika Muungano tulikubaliana baadhi ya mambo kufanya pamoja na sio Zanzibar kuwa Jimbo la Tnganyika. Alisema duniani kuna miungano mingi mizuri akiutolea mfano Muungano wa Uswis ambao una Serikali 24 na ule wa Muungano wa Maerkali wenye Serikali 52 na kusema kuwa ni uongo kuwa Serikali Tatu zitavunja Muungano na kusema Serikali Mbili ndizo zitakazovunja Muungano, na hata Muungano wa Serikali Tatu ukivunjika si kioja. Serikali Tatu hazitovunja Muungano Serikali Mbili ndizo zitakazo vunja Muungano. Alisema Uruhani wa Serikali ya Tanganyika ndio kero kubwa ya Muungano na Serikali tatu itairudisha Serikali ya Tanganyika ambako kero kubwa itakuwa ishatatuliwa.
Aliitaja Sheria ya Kuanzishwa na Bank Kuu ya Tanzania kuwa aliisaini Karume mwenyewe lakini Karume alipoona mapungufu ya Seria hiyo ndio maana akaanzisha PBZ. Aidha alisema kama Zanzibar inataka kuishtaki TFF itashinda na TFF haitokuwemo FIFA kwani TFF haiwakilishi Tanzania kama ilivyokuwa ZFA ilivyokuwa haiwakilishi Tanzania. Hivi hatuoni haya kubakia hivi hivi kuwa Manispaa wakati Zanzibar ilikuwa Empire alihoji Mwanasheria Mkuu na kuendelea kusema hivi tutamuamini vipi mtu ambae leo anasema Zanzibar si Nchi atakapokuwa Rais wa Tanzania ambao Zanzibar haitokuwa na Mamlaka atasema Zanzibar ni jimbo la Tanganyika na kumalizia kusema wengi wa Watanganyika wanachuki na Zanzibar. Aliwataka wanafunzi hao kuzungumzia mambo ya Muungano na kutaka kuwe na usawa “Bila ya kuwa na usawa katika Mungano huu huo si Muungano bali ni ukoloni” alisema, na kutaka kuwe na mfumo wa usawa katika Baraza la Mawaziri na Bunge na kuwe na makubaliano ya thuluthi mbili kila upande katika kupitisha sheria na kuengezwa au kupunguzwa mambo ya Muungano.
Alisema katika Muungano wa Serikali Tatu ni lazima Rasilimali zitumike kwa Usawa na sio kama hivi sasa Tanganyika inavyotumia Rasilimali za Muungano wao peke yao katika kusoma na kuinyima Zanzibar. Tume ya Pamoja ya Fedha haijaanza kazi mpaka leo, na katika Muungano kuna mapato ya Muungano na Matumizi ya Muungano na Mapato ya Muungano siku zote huwa mengi ambako Tnganyika hawataki tugawane. Alisema si kweli kama Muungano wa Serikali tatu una harama bali Muungano wa Serikali Mbili ndio wenye gharama na Zanzibar ndio inaharamika zaidi, aliwataka viongozi wawe wakweli na waache kuwapotosha wananchi. Aliwaonya Wazanzibar kuwacha kulumbana na badala yake kukaa pamoja kuidai nchi yao. Alisema Serikali ya Umoja wa Kitaifa iliundwa ili kuondowa tofauti kwa Wazanibar na kusema kuwa kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ni kuala gumu kuliko mabadiliko ya Muungano. Alisema Wanaotaka Seriakali Mbili hoja zao hazina msingi na hakuna haja ya kubakia kwenye Serikali mbili na wengi wanaotaka Serikali Mbili wanalinda maslahi yao ya kidunia.
Hoja yangu nawataka wanaotaka Serikali Mbili na Wanaotaka Mkataba wakae pamoja wajadiliano Mfumo wa Muungano wa Serikali Tatu mfumo ambao utakuwa na Mslahi na Zanzibar. Awali Mwenyekiti wa ZAHILFE alikanusha taasisi yake kuandaa kungamano la tarehe 6 mwezi wa 7 lililofanyika Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kingeni na badala yake kongamano hilo liliandaliwa na Mkowa wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vywa CCM na kusema Taasisi yake haina mafungamano na chama chochote cha siasa. Kongamano hilo lilianza na Wimbo wa Taifa wa Zanzibar na lilihudhuriwa na baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi. Marais 10 wa Serikali za Wanafunzi waliochangia katika Kongamano hilo walitaka Zanzibar yenye Mamlaka Kamili na Usawa Katika Muungano.
Chanzo: habari leo

No comments:

Post a Comment